Breaking News

CORONA : Waziri Mkuu Wa Uingereza Kukimbizwa Hospitalini Na Kulazwa

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amelazwa hospitalini ili kufanyiwa vipimo vya virusi vya corona, siku 10 baada ya kukutwa na virusi vya ugonjwa huo, ofisi yake ya Downing Street imesema.
Alikimbizwa katika hospitali moja ya mjini London siku ya Jumapili akionyesha dalili za virusi hivyo ikiwemo kiwango cha juu cha joto mwilini. Imedaiwa kuwa hatua hiyo ya tahadhari ilichukuliwa kutokana na ushauri wa daktari wake.
Waziri mkuu bado ndie msimamizi wa serikali, lakini waziri wa maswala ya kigeni nchini humo anatarajiwa kuongoza mkutano wa virusi vya corona siku ya Jumatatu.
Dkt. Sarah Jarvis, ambaye ni mtangazaji ,aliambia BBC kwamba bwana Johnson atafanyiwa vipimo kifuani na mapafu yake hususan iwapo amekuwa akipata tatizo la kupumua.
Alisema pia huenda akafanyiwa vipimo vya moyo wake pamoja na vipimo vingine kuhusu kiwango cha oksijeni mwilini na kile cha seli nyeupe za damu , ini na figo kabla ya kutolewa hospitalini.
Bwana Johnson alikuwa akifanya kazi kutoka nyumbani tangu alipotangazwa kwamba amekutwa na virusi vya corona tarehe 27 mwezi Machi.

No comments